Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupambana na vitendo vya ukeketaji yamefanyika Mjini Dodoma, huku Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh Ummy Mwalimu akiwa mgeni rasmi.
Maadhimisho hayo yalianza kwa maandamano yaliyoanzia viwanja vya Nyerere Square mpaka ukumbi wa Hazina Ndogo ambapo, Mh Ummy alitoa Tamko la msimamo wa serikali kuhusu ukatili wa ukeketaji na mipango ya Serikali ya awamu ya Tano kukabili ukiukwaji wa haki kutokana na vitendo hivi. |
0 Comments