Waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga amesema nchi hiyo haipo tayari kuwatambua wapenzi wa jinsia moja.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika eneo la bunge mjini Nairobi, Bw Odinga alisema suala la wapenzi wa jinsia moja lilitumiwa kama propaganda kupinga katiba mpya.
Waziri Mkuu huyo amesisitiza katiba mpya ya Kenya haikubali kuwepo wapenzi wa jinsia moja. Na amependekeza wapenzi hao wa jinsia moja wakamatwe na polisi endapo watajitokeza hadharani.
Lakini kauli hiyo imepingwa na David Kuria, mwanaharakati wa kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja.