
Pia wenye mashamba hayo nao watalipwa fidia ya mashamba na mali zao ili kuwapisha wakazi hao wa Kigilagila.
Awamu ya pili ya ulipaji wa fidia hiyo, inafuatia ile ya kwanza iliyohusisha bomoabomoa ya nyumba 293 katika eneo la Kipawa, jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kupisha upanuzi, kuboresha na kuongeza shughuli muhimu, zikiwamo zinazohusu usalama katika uwanja huo.
Tamko hilo lilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Leonidas Gama na Mhandisi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), William Shehambo, walipozungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti katika ofisi ya mkuu huyo wa wilaya jana.
0 Comments