
Blackburn Rovers imeiachia kisago Wolves kwa mabao 3-0. Davin Dunn, Brett Emerton na Ryan Nelsen wakifunga mabao hayo.
Chelsea imeendelea kujivuta baada ya kutoka sare ya 1-1 na Everton. Didier Drogba alifunga bao la Chelsea kwa njia ya mkwaju wa penati dakika tatu kabla ya mapumziko, huku bao la kusawazisha la Everton likifungwa na Jermaine Beckford katika dakika ya 86.
Nahodha wa Manchester City Carlos Tevez ameongoza kwa mfano, baada ya kuipatika timu yake bao pekee na la ushindi dhidi ya Bolton.
Na katika mchezo mwingine, Wigan imetoka sare ya 1-1 na Wigan. Mabao ya Wigan yamefungwa na Danny Collins wa Stoke aliyejifunga, na la pili Tom Cleverly. Magoli ya Stoke yamefungwa na Robert Huth na Matthew Ethrington.
Mchezo kati ya Blackpool dhidi ya Manchester United umeahirishwa kutokana na hali mbaya ya hewa kuathiri uwanja.
0 Comments