Aliwaagiza viongozi wa vijiji kuitisha mikutano ya vijiji na kuwaelimisha wananchi madhara ya kuuza chakula.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Adam Misana aliwataka wakulima kuhifadhi chakula kinachovunwa sasa kwa matumizi ya baadaye.
Misana alisema uzoefu unaonesha kuwa wakulima wengi huuza chakula chote na kisha kuhangaika.
Misana pamoja na mambo mengine alisema kitendo cha wakulima kuuza mazao yao sasa hakina faida kutokana na wanunuzi kuwanyonya kwa kuyanunua kwa bei ya chini.


0 Comments