Polisi nchini Norway sasa wanasema kuwa mtu aliyekuwa na bunduki aliyefyatua risasi katika mkusanyiko wa vijana katika kisiwa yenye kambi ya vijana nje ya mji mkuu, Oslo, Ijumaa jioni aliuwa watu wasiopungua 80.
Hatimaye mtu huyo alikamatwa kwenye kisiwa hicho, na polisi wanamhusisha piya na mripuko wa bomu katika jumba la ofisi za serikali katika mji mkuu, ambao uliuwa watu wengine 7.
0 Comments