Takriban waandamanaji watatu waliuawa kwenye mji mkuu Conakry nchini Guinea, baada ya majeshi ya usalama kuvunja maandamano ya upinzani.

Ripoti zinasema majeshi ya usalama yametumia mabomu ya kutoa machozi na marungu dhidi ya waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe mjini humo.
Guinea



Walitawanya maandamano yaliyokuwa yamepangwa na wanaounga mkono waandamanaji dhidi ya namna serikali inavyojiandaa kwa uchaguzi wa wabunge.


Raia wa Guinea walipiga kura ya uchaguzi wa rais Novemba iliyopita kwa mara ya kwanza tangu kupata uhuru mwaka 1958.

Lakini wanaofuatilia wanahofia kwamba demokrasia ya nchi hiyo inaweza ikawa hatarini.

Uchaguzi wa wabunge ulitakiwa ufanyike katika kipindi cha miezi sita lakini kwa sasa umepangwa kufanyika mwezi Desemba 29 na mamlaka husika pamoja na tume huru ya taifa ya uchaguzi (CENI).

Viongozi wa upinzani wanasema wanahofia uchaguzi utakuwa kama sarakasi.

Mkuu wa upinzani Cellou Dalein Diallo, ambaye alishindwa kwa kura chache katika uchaguzi mwaka jana, amemshutumu Rais Alpha Conde kwa kuweka ushirika wa karibu na mkuu wa CENI na kujaribu kuvuruga daftari la usajili wa wapiga kura.