Wakimbizi wote wenye asili ya Kisomali nchini Kenya, wameamriwa
kuondoka katika maeneo ya mijini na kurudi kambini baada kuwepo kwa milipuko ya
mara kwa mara.
Misaada haitatolewa tena kwa yeyote ambaye atakuwa mjini, amesema mkuu wa
shirika la wakimbizi la umoja wa mataifa.
Misaada haitatolewa tena kwa yeyote ambaye atakuwa mjini, amesema mkuu wa
shirika la wakimbizi la umoja wa mataifa. Milipuko hiyo imekuwa ikitokea mara kwa mara katika maeneo yenye idadi kubwa
ya watu wenye asili ya Kisomali, kama vile mkoa wa Kaskazini Mashariki na mtaa
wa Eastleigh iliyoko mjini Nairobi. Mashambulizi hayo yanaaminika kufanywa na watu wanaoaminika kuwa wanachama
cha kundi la Kiislamu la Al Shabab.
0 Comments