Madereva taxi nchini Ubelgiji leo wamefanya mgomo baridi kuipinga serikali kwa baadhi ya masharti mapya ambayo kwa upande wao wameona kama ni uonevu.Maandamano hayo ambayo yamesababisha usumbufu mkubwa katika baadhi ya barabara kubwa jijini Brussel.
Muungano wa madereva taxi nchini Belgium (ATB) wanasema hawawezi kukubali katiba ambayo inaweka sheria kadhaa ambazo zinawapa ugumu wa kazi.Wanasema, kwa mfano, kwamba wanapaswa kuvuta sigara ndani ya gari zao kitu ambacho wamekipinga vikali.Pichani madereva hao wakiwa wameyapanga magari yao barabarani kuendeleza mgomo huo.