Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akikiongoza Kikao cha Kamati ya Taifa ya Maadhimisho ya Sherehe na Mapambo akiwa mwenyekiti wa Kamati hiyo kilichofanyika Jumba la Wananchi Forodhani Mjini Zanzibar. Kikao hicho kilikutana kupokea tathmini ya Sherehe zilizopita za Miaka 49 ya Mapinduzi yua Zanzibar pamoja na maandalizi ya nusu karne ya Maadhimisho ya Sherehe zijazo za Mapinduzi.

  Mkurugenzi wa Idara ya Maafa Zanzibar Nd. Juma Ali Hamad akiwasilisha Taarifa juu ya muelekeo wa mvua za masika mwezi Machi hadi Mei kwenye kikao cha Kamati ya Maafa Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Kanda ya Zanzibar Nd. Khamis Suleiman akitoa ufafanuzi  kwa wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Maafa Zanzibar juu ya hali iliopo ya muendeleo wa Mvua za Masika zinazonyesha Nchini kwenye ukuimbi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar uliopo Vuga Mjini Zanzibar.Picha na Hassan Issa wa  - OMPR – ZNZ.