Stori:Imelda Mtema
Baada ya hivi karibuni msanii wa filamu Bongo, Wema Sepetu kumlipia Kajala Masanja faini ya shilingi milioni 13 ili asiende jela kwa kesi iliyokuwa ikimkabili, Kajala ameamua kulipa fadhila kwa kujichora tatuu ya jina la Wema mgongoni mwake.

Akizungumza na Ijumaa juzi kuhusiana na uamuzi huo, Kajala alisema Wema amemfanyia kitu kikubwa sana kiasi kwamba amefikiria cha kumlipa bila majibu hivyo akaamua kujichora tatuu hiyo ambayo itamfanya amkumbuke daima.“Kwa kweli Wema amenifanya kitu kikubwa sana, nyie wenyewe ni mashahidi. Nimefikiria nimlipe nini kwa fadhila zake hizo, nikakosa jibu na ndipo nikaamua kujichora tatuu hii ambayo haitafutika mwilini mwangu maisha,” alisema Kajala.