Msanii Bora wa Hip Hop 2013, Joseph Haule 'Profesa Jay'.

Msanii Young Killer aliyechukua tuzo ya msanii bora chipukizi wa Hip Hop 2013.

WASANII wanaofanya vizuri zaidi katika muziki wa Hip Hop nchini, Joseph Haule 'Profesa Jay' na Young Killer wamefanikiwa kutwaa tuzo katika tamasha la Usiku wa Hip Hop lililofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Dar es Salaam. Young Killer amechuka tuzo ya msanii Bora Chipukizi wa Hip Hop kwa wimbo wake wa 'Dear Gambe' aliomshirikisha msanii Belle 9. Washindi hao wamewabwaa wasanii wenzao kibao waliokuwa wanawania tuzo hizo.