Mshiriki wa Tanzania aliyetolewa kwenye shindano la Big Brother 'The Chase' Feza Kessy,  atawasili nchini leo (Jumatano) jioni saa kumi na mbili na nusu kwa ndege ya South African Airways. Feza aliondolewa katika shindano la la Big Brother 'The Chase' Jumapili iliyopita na kuungana na Mtanzania mwenzake Ammy Nando aliyetangulia kutoka katika jumba hilo. Wadau mnaombwa kujitokeza kumpokea mshiriki wetu.

Feza Kessy