Stori: Brighton Masalu
MWIGIZAJI mahiri Bongo, Wastara Juma Issa Abeid ‘Wastara’ amesema suala la kuolewa tena halikwepeki licha ya kutokuwa na mawazo juu ya suala hilo kwa sasa.Akizungumza na paparazi wetu, Wastara ambaye ni nadra sana kukosea awapo mbele ya kamera, alisema yeye kama mwanamke aliyekamilika hadhani kama atakaa bila mwanaume lazima ataolewa tena.
“Mimi ni mwanamke niliyekamilika, suala la kuolewa ni lazima, japo kwa sasa sifikirii kufanya hivyo, lakini sidhani kama nitaweza kukaa bila mwanaume, lakini pia usumbufu kutoka kwao unaendelea,” alisema Wastara