Stori: Hamida Hassan
STAA wa majanga, Snura Mushi ameuanza mwaka 2014 vibaya kutokana na maradhi ya presha yanayomsumbua mara kwa mara

Snura Mushi.
Akipiga stori na Ijumaa Wikienda, Snura alisema kuwa hajui ni kitu gani kinamsumbua lakini kila akienda kupima anaambiwa ni presha imepanda na vidonda vya tumbo.
“Nimekuwa nikiumwa mara kwa mara na nikishikwa ni lazima niwekewe drip kwani naishiwa nguvu nakosa raha pia, sijielewi ingawa naambiwa kuwa nina mawazo,” alisema Snura akiwa nyumbani kwake, Mwananyamala, jijini Dar.