Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Human Rights Watch linasema kuwa zaidi ya raia 2,000 wameuawa nchini Nigeria mwaka huu na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.

Kwa mujibu wa shirika hilo, vifo hivyo vimetokea katika mashambulizi 95 tofauti katika zaidi ya miji 70 na vijiji kaskazini mashariki mwa taifa hilo.
Rais Goodluck Johnathan amepata shinikizo la kusitisha mashambulizi hayo na kuwaokoa zaidi ya wasichana 200 wa shule waliotekwa nyara miezi mitatu iliopita.
Anatarajiwa kukutana na baadhi ya familia za wasichana hao kufuatia ombi la mwanaharakati wa Pakistan Malala Yousafzai ambaye alikutana naye hapo jana.