Kiongozi wa waasi wa Uganda LRA,Joseph Konyi
Dominic Ongwen, mmoja kati ya makamanda aliyekuwa na cheo kikubwa katika jeshi la waasi wa Uganda Lord Resistance Army (LRA) ambaye pia alikuwa mtu wa karibu sana na Joseph Kony, inataarifiwa amejisalimisha kwa kikosi cha jeshi la Marekani kilichoko Africa ya kati ,na hii ni kwa muujibu wa msemaji wa kikosi cha Marekani nchini humo.
Dominic alitekwa nyara na LRA alipokuwa na umri wa miaka 10, na alikuwa akipanda vyeo katika jeshi hilo la waasi na amekuwa akisakwa na mahakama ya uhalifu wa kivita kwa makosa kadhaa yakiwemo ya mauaji ,uporaji,pamoja na utumikishaji.