Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (katikati) akimsikiliza Mwakilishi
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez (kulia), wakati kiongozi
huyo alipomtembelea Waziri huyo ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kujadiliana masuala
mbalimbali ya ushirikiano kati ya Wizara yake na ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN) nchini.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi wa Wizara hiyo, Harrison Mseke, anayefuata ni
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) nchini, Joyce
Mends-Cole.
0 Comments