wagombea wa uraisi ishirini kati ya thelathini katika jamhuri ya afrika ya kati wametoa wito wa kura zilizopigwa kufutwa kwa madai ya kuwepo kwa ulaghai.
Matarajio yalikuwa baada ya uchaguzi jumatano hali ya amani ingeweza kurudi nchini humo ambako maelfu wamefariki dunia katika vita vya kidini.

kura zaidi ya robo zimehesabiwa, waziri mkuu wa zamani , faustin archange touadera, ndio anaongoza mpaka sasa. msemaji wa kundi la wagombea hao ishirini , théodore kapou , amewaambia waandishi wa habari kuwa hawawezi kukubali njia za uendeshaji uchaguzi .
"Sisi , wagombea kwa uchaguzi wa urais, watia sahihi wa tamko hili, tunakataa ushirika wa uchaguzi batili kama huu, Tunatangaza kuwa mchakato wa uchaguzi ' si wa kuaminika ' . Ni lazima usimamishwe ili ushirikiano uwepo na utekelezwaji uendele.