Home
Home
About
Contact
Home
Mwanamke atolewa hai kwenye vifusi Nairobi
Mwanamke atolewa hai kwenye vifusi Nairobi
MAGANGA ONE.
May 05, 2016
Mwanamke ametolewa akiwa hai kutoka kwenye vifusi siku sita baada ya jumba kuporomoka katika mtaa wa Huruma, Nairobi.
Juhudi za uokoaji bado zinaendelea ingawa kuna wasiwasi kwamba muda wa kupata manusura wakiwa hai unayoyoma.
Image caption
Jengo hilo liliporomoka baada ya mvua kubwa kunyesha Ijumaa
Kwa mujibu wa Pius Masai, mkuu wa kitengo cha taifa cha kukabiliana na majanga, idadi ya waliofariki kufikia sasa imefikia 36.
Mtoto mchanga atolewa kwenye vifusi Nairobi
Watu 136 wameokolewa wakiwa hai lakini watu 70 kufikia sasa bado hawajulikani walipo.
Siku mbili zilizopita, mtoto wa umri wa miezi sita aliokolewa baada ya kukaa kwenye vifusi kwa siku nne.
Msichana huyo alitolewa kwenye vifusi mwendo wa saa kumi usiku na kupelekwa hospitalini.
Image caption
Maafisa wa uokoaji bado wanawatafuta manusura zaidi
Alipatikana akiwa amefunikwa kwa blanketi ndani ya ndoo na hakuonekana akiwa na majeraha yoyote.
Babake mtoto huyo, Bw Ralson Wasike, akihutubia wanahabari baadaye, alisema bintiye amekuwa na nguvu sana.
BBC
Post a Comment
0 Comments
Social Plugin
Facebook
Tags
Contact form
0 Comments