Maafisa nchini Somalia wanasema kuwa mtu anayeaminika kupanga mashambulio ya chuo kikuu cha Garissa miaka miwili iliopita ameuawa.
Mohamed Kuno aliuawa pamoja na watu wengine wanne na maafisa wa usalama Kusini mwa Somalia.

Serikali ya Kenya inasema kuwa Kuno ndiye aliyepanga mauaji ya chuo kikuu cha Garissa ambapo takriban watu 148 na wapiganaji kutoka kwa kundi la wapiganaji kutoka Somalia al-Shabab.
Image copyrightB
Image captionGarissa
Kuno,ambaye ni raia wa Kenya alielekea Somalia na pia alilaumiwa kwa mashambulio kadhaa ya kikosi cha wanajeshi wa Kenya wanaokabiliana na al-Shabab.
Serikali ya Kenya ilitoa zawadi ya zaidi ya dola 200,000 kwa mtu atakayemkamata kufuatia shambulio hilo la Garissa.