DJ raia wa Afrika Kusini ambaye pia ni producer maarufu kama Black Coffee, amewabwaga wanamuziki maarufu wakiwemo WizKid, Yemi Alade na Diamond Platnumz na kushinda tuzo la kimataifa la usanii la BET.

Mwaka uliopita Black Coffee alitoa albamu yake ya tano, Pieces of Me, na kupata mashabiki wengi.
Mwaka 2015 na 2016 umaarufu wake uling'aa katika ulingo wa kimataifa maeneo tofauti kote duniani
Tuzo hilo llitangazwa kupitia kwa mitandao ya kijamii.