Kikosi kigumu na bora cha timu ya Mol kikipata picha ya pamoja kabla ya mpambano kuanza.
Timu ngumu ambayo inaendeleza ubabe kila mara kwa timu zote za kiafrika nchini Ubelgiji Mol Fc jana iliendeleza vyema shughuli zake za kukata kilimilimi kwa timu zote zilizo na uwezo wa chini kimchezo kwa kuwafundisha Antwerpen Fc soka baada ya kuirarua kwa jumala ya goli 4-3 katika uwanja wa Antwerpen.
Mol ina kila sababu ya kuwa timu bora kwa kujidhihirishia jana pale ilipoifunga Antwerpen Fc ikiwa ni mara ya tatu mfululizo.
Ikicheza kwa kujiamini zaidi Mol Fc ilicheza mchezo mzuri sana na kila mmoja aliyekuwepo uwanjani pale alikisifia kikosi hicho.Antwerpen hii ni mechi yao ya pili sasa kupoteza,kabla ya mechi ya jana ilibugia goli 5-3 toka kwa Mavetarani wa Antwerpen.
Mara baada ya mchezo kumalizika Uongozi wa Mol Fc ulitangaza kutaka mechi na vijana wa Holland kwani kwa hapa Ubelgiji timu zote kama Antwerpen, Leuven na Liege wote walishachezea vichapo kila walipokutana na Mol Fc. |
0 Comments