Jimmy Luhende, Mkurugenzi wa Taasisi ya Utawala Bora na Demokrasia nchini (ADLG), akizungumza katika Mjadala wa Mwezi June uliofanyika hii leo Jijini Mwanza. 

Taasisi ya ADLG huendesha mijadala tofauti tofauti kila mwisho wa mwezi ambapo wadau mbalimbali hukutana na kujadili mada husika. Mjada wa mwezi june umeangazia Fursa, changamoto na athari za kimazingira zitokanazo na shughuli za migodini.


Katika mjada huo, wadau wameishauri serikali kupia Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEC, kuboresha sheria ya usimamizi wa mazingira ili kuweza kuwafanyia tathmini za uchafunzi wa mazingira wachimbaji wadogo kwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakichangia uchafunzi wa mazingira nchini.
Jamal Baruti ambae ni Mratibu wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC, Kanda ya Ziwa, akiwasilisha mada juu ya tathmini ya athari za mazingira zitokanazo na shughuli za uchimbaji wa madini.

Amesema tathimini ya uchafuzi wa mazingira imekuwa ikifanyika kwa wachimbaji wakubwa wa madini kabla na baada ya uchimbaji lakini wachimbaji wadogo wamekuwa hawaguswi na tathmini hiyo kutokana na kutojumuishwa katika tathimini hiyo kwa mjibu wa sheria ya mazingira.
Mmoja wa washiriki akichangia mada
Mmoja wa washiriki akichangia mada
Mdau wa Mazingira, Sheikh Saad Rwekaka ambae pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu BAKWATA mkoani Mwanza, akitoa maoni yake. Anasema ni vyema wachimbaji wadogo wadogo wakashirikishwa ipasavyo ili kuondokana na uchafuzi wa mazingira katika shughuli zao.
Mmoja wa washiriki akichangia mada
Wadau wa Mazingira
Wadau wa Mazingira
Wadau wa Mazingira
Mijadala ikiendelea
Wadau wa Mazingira
Wadau wa Mazingira
Wadau wa Mazingira
Wadau wa Mazingira
Ashraph Omary (katikati) ambae ni mdau wa Mazingira kutoka taasisi ya MEDTO (Mining and Environmental Transformation for Development Organisation), akifanyiwa mahojiano na mwanahabari. 
Imeandaliwa na BMG