Bi Wassermann Schultz anatarajiwa kujiuzulu baada ya kumalizika kwa kongamano la kuidhinisha mgombea. Anatarajiwa kufungua na kufunga kongamano, na pia atahutubu.
Rais Barack Obama amemshukuru kwa mchango wake kwa chama.

Hayo yakijiri, Bw Sanders na wafuasi wake pia wameeleza kusikitishwa kwao na hatua ya Bi Clinton kumteua Seneta wa Virginia Tim Kaine kuwa mgombea mwenza wake.
Badala yake, walitaka mtu anayeegemea zaidi siasa za mrengo wa kushoto.
Hata hivyo, Bw Sanders alisema: “Nimemfahamu Tim Kaime kwa miaka kadha … Tim, ni mtu mwerevu, mwerevu sana. Ni mtu mzuri.”
Bi Clinton alipigwa jeki Jumapili baada ya meya wa zamaniwa New York, aliyechaguliwa kupitia chama cha Republican, Michael Bloomberg, kumuunga mkono.
Kongamano la chama cha Democratic litaanza Jumatatu kwa hotuba za Mke wa Rais Michelle Obama na Bw Sanders.
Kongamano hilo litaendelea kwa siku nne, na limeandaliwa baada ya kongamano la chama cha Republican kumuidhinisha Donald Trump wiki iliyopita.