Mkutano wa mawaziri wa fedha wa mataifa ya G20, umemalizika nchini China, huku onyo likitolewa kuwa, kura ya maoni iliyoifanya Uingereza kujiondoa ndani ya muungano wa mataifa ya Bara Ulaya, imesababisha hatari kubwa zaidi na kuyumbisha uchumi wa Dunia.

Mkutano huo wa G20 umesema kwamba kuna hatari kubwa kuwa, mazungumzo kuhusiana na hatua hiyo ya Uingereza yakaibua uchungu mwingi.
Lakini viongozi hao wakasema kuwa EU imejiandaa ipasavyo kushughulikia tatizo hilo huku wakisema kuwa wana matumaini makubwa kuwa Uingereza sharti iendelee kuwa mshirika mkubwa wa EU.