MakondaMkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Dar es Salaam
KUTOKANA na kuongezeka kwa vitendo vinavyoashiria kuwepo kwa watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametangaza operesheni ya kuwasaka wanaume wanaojihusisha na tabia hiyo mbovu ya ‘mashoga’ jijini humo ilihali wakijua ni kinyume cha sheria za nchi.
Makonda amesema vitendo hivyo vimeanza kuongezeka jijini humo na lengo lake ni kuwaokoa watoto wasiige mambo hayo yanayoonekana kukua kwa kasi.
Mkuu huyo wa Mkoa amesema, “hili ni tatizo linalokua kwa kasi sitaruhusu liendelee katika mkoa wangu, nitawasaka popote walipo”.
“Hata hapa bandari wanaweza kuwapo mashoga wafichueni, mkiona mtu ana tabia za ajabu ajabu mfichueni, tutashughulika nao”.