mbuzi kazaa binadamu 
Nigeria
HAYA ni maajabu mengine kuwahi kutokea duniani! Mbuzi alyekuwa na mimba amejifungua kiumbe ambacho kina sura kama ya binadamu.
Tukio hilo lilitokea jana Jumatano katika mji wa Taraba nchini Nigeria na kuwaacha watu midomo wazi wakishangaa huku wasiamini kilichotokea.
Chombo cha habari cha Rariya cha nchini humo kiliripoti kuwa, kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio  hiyo, huenda mwenye mbuzi huyo alifanya naye mapenzi, ndiyo maana akazaa mbuzi mwenye sura ya binadamu.
Baada ya tukio hilo kutokea na taarifa kusambaa mjini na kwenye mitandao ya kijamii nchini humo, hakuna mtu yeyote mpaka sasa aliyejitokeza na kukiri kuwa mbuzi yule ni wake, na inadaiwa mara baada ya kujifungua kiumbe hicho kilipoteza uhai muda mfupi baadaye.