Watu 19 wameripotiwa kuuwawa nchini Japan baada ya mtu mmoja kuwashambulia kwa kisu katika kituo kimoja cha walemavu, kilichoko katika mji wa Sagamihara, magharibi mwa mji mkuu Tokyo. Zaidi ya watu 20 wamejeruhiwa.

Ripoti nchini Japan zinasema kuwa mtu mmoja ambaye alikuwa akifanya kazi katika kituo hicho, alijipeleka hadi kituo cha polisi na kukiri kuwa ndiye aliyetekeleza mauwaji hayo ya kutisha.