Timu ya waokoaji katikati ya Italia inajitahidi kuendelea kuokoa maisha ya watu ambao bado wako hai kufuatia tetemeko la Ardhi lililoathiri miji mitatu na kuua watu zaidi ya 250.
Mamia ya wengine wamejeruhiwa.
Upekuzi ambao umefanywa kwa siku mbili unakwamishwa na mishindo yenye nguvu.
Mshindo mkubwa ni ule uliotokea katika mji wa Amatrice ambapo waokoaji walikimbia kutokana na kuangukiwa na uchafu.
Serikali ya Italia imetangaza hali ya hatari kwa maeneo yaliyokubwa na tetemeko la ardhi na kutangaza kutoa euro milioni hamsini kutoka mfuko wa dharura.
0 Comments