Ripoti kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC zinasema kuwa wanajeshi wamepata miili ya takriban raia 30 waliouawa katika shambulizi mashariki mwa taifa hilo.

Msemaji wa jeshi Mark Azuray ameambia shirika la habari la AFP kuwa mauaji hayo yalitokea katika mji wa Beni nyakati za usiku.
Wanajeshi wanashuku kuwa kundi la wanamgambo la ADF lilitekeleza mauaji hayo.
ADF ni kundi la kujihami lililo na asili yake nchini Uganda, na linaendeleza shughuli zake karibu na mpaka.