Doto James
Rais Dkt. John Magufuli amemteua, Doto James kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.
Taarifa ya Ikulu jijini Dar es Salaam imesema kabla ya uteuzi huo Doto James alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango (Sera).

Doto James ataapishwa Septemba Mosi, 2016 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo kufuatia uteuzi huo aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile atapangiwa kazi nyingine.