Kwa mara nyingine tena, tetemeko baya la ardhi, limegonga maeneo ya katikati mwa Italia, mahali ambapo watu 300 waliuwawa mwezi Agosti mwaka huu.
Taarifa za awali zinasema kuwa uzito wa tetemeko hilo limefikia 6.6 katika vipimo vya Richa.

Watalamu wa majanga ya dharura wanasema kuwa eneo la kusini mashariki mwa mji wa Perugia limekuwa kitovu cha mtetemeko huo.
Uzito wa tetemeko hilo limesikika umbali wa kilomita 150 hadi mjini Roma.