Somalia imeimarisha mchakato wa uchaguzi unaolenga kuwachagua wawakilishi wa bunge jipya la taifa hilo.
Jumla ya wajumbe 14,000 walioteuliwa watapiga kura kuwachagua wabunge 275 .

Umoja wa Mataifa una imani kwamba hatua hiyo ni muhimu kuelekea chaguzi zijazo za taifa hilo ambapo raia wa Somalia watashiriki shughuli hiyo moja kwa moja ifikapo mwaka 2020.
Taifa hilo lililozongwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa miongo kadhaa linatarajiwa kufanya uchaguzi wa Urais mwishoni mwa mwezi ujao wa Novemba