Bingwa wa urushaji mkuki Afrika, Julius Yego, alinusurika baada ya gari lake kuhusika kwenya ajali ya barabarani mjini Eldoret, magharibi mwa Kenya.
Yego, ambaye alishinda fedha katika urushaji mkuki michezo ya Olimpiki Rio de Janeiro, Brazil, ameandika kwenye Facebook kwamba yupo katika hali nzuri.

"Mungu anaishi na ni mkuu! Niko salama watu wangu. Siamini kwamba niko hai. @mungu yupo! Nimo katika hali nzuri," Yego ameandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.
Picha za gari lake, ambalo limeharibiwa vibaya sehemu ya mbele, zimekuwa zikisambazwa sana mitandaoni Kenya.
Mashabiki wake wamekuwa wakimpa pole na kumtakia afueni ya haraka.
Julius YegoImage copyrightJULIUS YEGO / FACEBOOK
Yego alijifunza urushaji mkuki kwa kutumia video kwenye YouTube na kumfanya apewe jina 'Mwanariadha wa YouTube'.
Alishindwa ubingwa wa dunia wa urushaji mkuki wa IAAF mwaka 2015