Kundi la kigaidi la Al-Qaeda limethibitisha kuuawa kwa kiongozi wao mkubwa Farouq al-Qahtani huko kaskazini Mashariki mwa Afghanistan katika mapigano na vikosi vya marekani mwezi mmoja uliopita.

Huko mjini Washington wamethibitisha kifo hicho kutokea November 15 yalikuwa ni makabiliano adhimu.
Lakini Al-Qaeda wamesema kuwa mkewe na watoto waliuwawa pia japo hawakujulikana kijeshi.
Vikosi vya Marekani vimeiweka Al-Qahtani mzaliwa wa Saudi huko Quatar kama mtu wanayemtafuta sana kwao akituhumiwa kuhusika na mipango ya mashambulizi huko Marekani na Ulaya