Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akizungumza na vyombo vya habari, wakati akikanusha taarifa zinazoenezwa mitandaoni kuwa Benki hiyo iko mbioni kufunga baadhi ya matawi yake kwa madai kuwa imeyumba kiuchumi. Dkt. Kimei amekanusha taarifa hizo kwa kusema si ukweli na sasa wako kwenye mikakati ya kufungua matawi mengine 11 kabla ya Januari 2017.