Wazimbabwe si watu wa kutaka pesa zao kuchezewa hasa baada ya kuzinduliwa kwa noti ,mpya ambazo zina lengo la kusuluhisha tatizo la uhaba wa pesa nchini humo.
Picha za watu wakiwa wamelala nje ya mabenki wakisubiri yafunguliwe ili watoe pesa zao zimekuwa zikichapishwa kwenye mitandao ya kijamii.

Gavana wa benki kuu Jonathan Moyo, alisema mwezi Mei kuwa noti hizo zitadhaminiwa na mkopo wa dola milioni 200 kutoka benki ya Africa Export-Import
Noti hizo za dola 5, 10, 20 zitakuwa na thamani sawa na zile wanazotumia za Marekani.
Zimbabwe ilianza kutumia dola za Marekani ilipoacha kutumia sarafu yake mwaka 2009.
Tangu wakati huo wazimbabwe wamekuwa wakitumia dola pamoja na sarafu za nchi zingine ikiwemo ya Afrika kusini ya rand na ya China ya yuan.