Kamanda Ras Makunja wa Ngoma Africa band uso kwa uso na Paparazi !

Usiku wa manane katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa J.K.Nyerere jijini
Dar es salaam jana usiku jicho la kamera ya paparazi lilimzoa mwanamuziki
Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja ambaye alikuwa ndio kwanza katua kutokea nchini Ujerumani,mwanamuziki huyo wa kimataifa anayeiongoza bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa Band aka FFU Ughaibuni,alipokumbana na paparazi akutaka maneno zaidi
bali alipakiwa katika gari moja jeusi aina na Noa na kutokomea aliko tokomea,ubuyu umedokeza kuwa bendi hiyo ipo likizo kwa muda wa miezi miwili ,likizo hiyo imetokana na kufanya tour miaka miwili bila mapumziko,
Kiongozi huyo wa Ngoma Africa band inawezekena yupo nyumbani Tanzania labda kwa likizo kama inavyodhaniwa,Any way Kikamanda  Ketu Ras Makunja karibu nyumbani,