Mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange akiongea na Mbunge wa Mafia Mhe. Mbaraka Dau  wakiwa katika  ziara ya kikazi ya siku mbili  kisiwani Mafia mkoa wa Pwani. 

Picha na Ofisi ya Mbunge.
Mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange amefanya ziara ya kikazi ya siku mbili  kisiwani Mafia mkoa wa Pwani. Pamoja na mambo mengine Jenerali Mwamunyange ametembelea gati la Kilindoni Mafia na visiwa vidogo vya Shungimbili, Nyororo na Mbarakuni na kujionea shughuli zinazoendelea hapo. Pichani anaonekana Mbunge wa Mafia Mhe. Mbaraka Dau (fulana ya mistari) akitoa maelezo ya jinsi wananchi wanavyopata huduma katika gati la Kiindoni