Image result for WAFANYABIASHARA WA MADUKA ARUSHA





Na Woinde
Shizza,Arusha



WAFANYABIASHARA wa maduka jijini Arusha,wameilalamikia halmashauri

hiyo ,wakipinga notisi ya miezi mitatu waliopewa ,inayowataka kuondoka

katika maduka hayo,ifikapo Machi 30,mwaka huu, kufuatia maduka yao

kudaiwa kumilikiwa ma madalali na hivyo kuikosesha  mapato
halmashauri

hiyo .





Aidha walidai kuwa hawapo tayari kuhama na hawatambuni notisi hiyo na

wataendelea kufanyabiashara zao kama kawaida kwa kuwa wamekuwa

wakilipa mapato ya halmashauri kama inavyopaswa.



Wakizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari,uliolenga kujadili

notisi hiyo, mwenyekiti wa wafanyabiashara hao jijini Arusha,Loken

Masawe alisema halmashauri hiyo imetoa notisi kwa lengo la kutangaza

tenda kwenye maduka hayo ,hatua hiyo walisema haiwatendei haki kwani

wengi wao  walijenga maduka hayo na hatua hiyo itawasababisha

washindwe kulipa fedha walizokopa kwenye mabenki mablimbali.



‘’Sisi hatujakataa tenda wanayotaka kutangaza kwenye maduka hayo ila

kwanini wanataka kuweka watu wao ili sisi tufe njaa ,familia zetu

tutazilisha nini ,tunachosema tenda hii sio halali na

hatutakubali’’alisema Masawe





Wafanyabiashara hao  ambao ni zaidi ya 1200 wanaomiliki maduka katika

maeneo mbalimbali katika jiji hilo,walienda mbali zaidi kwa kumtaka

rais John Magufuli kuingilia kati ili kuwanusuru na kadhia hiyo

inayolenga kuwadhalilisha wao na familia zao





Naye mfanyabiashara Meja willson Lukumamu alisema kuwa walijenga

maduka katika eneo la stand ndogo kwa gharama zao ,wakati huo eneo

hilo lilikuwa pori na kwamba hadi sasa hawakuwahi kurejeshewe gharama

zao .



‘’Huu mpango unaofanywa na manispaa ni batili kwani sisi kama

wafanyabiashara hatujawahi kushirikishwa ,tunachotaka usitishwe na

biashara zetu ziendelee kama kwaida’’alisema





Akizungumzia malalamiko ya wafanyabiashara hao,Meya wa jiji la

Arusha,Kalisti Lazaro alisema kimsingi madai yao hayana msingi, kwani

mpango huo ni utekelezaji wa maoni ya tume iliyoundwa na mkuu wa mkoa

wa Arusha,Mrisho Gambo iliyolenga kuchunguza uhalali wa umiliki wa

maduka hayo.



Kalisti alisema kuwa halmashauri hiyo haitarudi nyuma katika mpango

huo kwani imekuwa ikipozeza zaidi ya shilingi bilioni 2.1 kutokana na

maduka hayo kumilikiwa na madalali ambao huwapangishia wafanyabiashara

kwa gharama kubwa huku halmashauri hiyo ikipata mapato kiduchu.



‘’Baada ya tume kuundwa  na mkuu wa mkoa ,Mrisho Gambo
ilifanyakazi ya

kuchunguza uhalali wa umiliki wa maduka hayo na kubaini kuwa wamiliki

wa maduka hayo wengi wao ni madalali na wamekuwa wakipangisha maduka

hao kwa gharama kubwa na kuilipa halimashauri kiwango kidogo’’alisema

Meya







Alitolea mfano mfanyabiashara Morice Makoi kuwa anamiliki maduka 27

,eneo la kituo cha daladala na amepangisha kwa shilingi laki tano hadi

laki nane kwa  duka moja huku yeye akiilipa halmashauri hiyo shllingi

50,000 kwa mwezi,jambo ambalo alisema halikubaliki.



Alisisitiza kuwa halmashauri hiyo haina mpango wa kuwafukuza

wafanyabiashara hao ila inachofanya ni kutangaza tenda upya ili kila

mmoja aweze kuomba umiliki na atakayeshinda atakabidhiwa duka lake kwa

mkataba maalumu .



Aliwataka wafanyabiashara hao kuacha kulalamika badala yake wafuate

taratibu ikiwemo kuleta maombi mapya ya barua yatakayoambatana na TIN

namba,Lesen,na kwamba watakao kidhi vigezo hivyo watakabidhiwa duka

mara moja.