Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akisisitiza jambo wakati wa kikao baina yake na mwekezaji kutoka Denmark, Malte Meyer (katikati), aliyemtembelea ofisini kwake Dodoma hivi karibuni na kueleza nia ya kuwekeza kwenye sekta ya nishati nchini. Kulia ni Ofisa kutoka Ubalozi wa nchi hiyo, Derrick Katunzi. 

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na mwekezaji kutoka Denmark, Malte Meyer (kushoto) na Ofisa kutoka Ubalozi wa nchi hiyo, Derrick Katunzi (kulia).

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akimsikiliza mwekezaji kutoka Kampuni ya L&T ya India, Sanjay Gupta (kulia). Katikati ni Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi Hillary.

Kutoka kulia ni Mkuu wa Sekta inayoshughulikia masuala ya umma katika Benki ya Stanbic, Noella Kimaro, Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo, Thomas Buonga na Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi Hillary, wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), walipomtembelea ofisini kwake Dodoma hivi karibuni na kueleza nia yao ya kuwekeza katika sekta ya nishati nchini.

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto), akiagana na Ujumbe kutoka Benki ya Stanbic, waliofika ofisini kwake mjini Dodoma, kueleza nia yao ya kuwekeza katika sekta ya nishati nchini. Kushoto kwa Waziri ni Mbunge wa Sumbawanga, Aeshi Hillary.

Na Veronica Simba - Dodoma

Wawekezaji
mbalimbali wamemtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter
Muhongo, ofisini kwake mjini Dodoma na kumweleza nia yao ya kuwekeza
kwenye miradi mbalimbali katika sekta ya nishati nchini.

Akizungumza
na Waziri Muhongo, mwakilishi wa Kampuni ya L&T ya India, Sanjay
Gupta aliwasilisha nia ya Kampuni hiyo ya kujenga njia ya kusafirisha
umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi
Mkuu wa Benki ya Stanbic, Thomas Buonga akiwa ameambatana na Mkuu wa
Sekta inayoshughulikia masuala ya Umma wa Benki hiyo, Noella Kimaro,
walimweleza Waziri kuwa wanaangalia fursa ya kuwekeza katika miradi ya
sekta ya nishati.

Naye, mwekezaji kutoka Denmark, Malte Meyer,
akiwa amefuatana na Ofisa kutoka ubalozi wa nchi hiyo, Derrick Katunzi,
alisema nia ya kampuni yake ni kuwekeza katika sekta ya nishati hususan
uzalishaji wa umeme kwa kutumia upepo.

Waziri Muhongo
aliwakaribisha wawekezaji hao na kuwahakikishia kupata ushirikiano
kutoka serikalini endapo watakidhi vigezo stahiki vya uwekezaji
vilivyowekwa.