Aliyekuwa rais wa klabu ya Barcelona Sandro Rosell amekamatwa kufuatia uchunguzi wa ulanguzi wa fedha.
Baadhi ya watu wengine pia walikamatwa baada ya polisi kuvamia ofisi tisa na nyumba kaskazini mashariki mwa Catalonia.

Hatua hiyo nio miongoni mwa haki za mauzo zinazoshirikishwa na Brazil kulingana na duru za maafisa wa polisi.
Rosell alikuwa rais wa Barcelona kutoka mwaka 2010 hadi 2014, wakati alipojiuzulu kufuatia uamuzi wa mahakama ya Uhispania kuchunguza usajili wa mchezaji wa Bacelona Neymar mwaka 2013.
Mnamo mwezi Juni 2016, Barcelona ililipa faini ya Yuro milioni 5.5 kufuatia uhamisho wa mchezaji huyo kutoka klabu ya Santos.
Klabu hiyo ilishutumiwa kwa kukwepa kulipa ushuru, swala inalokana.
Mke wa Rosell ni miongoni mwa wale waliokamatwa siku ya Jumanne.