Meneja Masoko wa Benki ya Finca, Nicholous John katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa udhamini  wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 5 na Klabu ya soka ya Dar City F.C. Kulia ni Rais wa Klabu hiyo Azimkhan Akber Azimkhan na Mwenyekiti wa Chama cha Soka  mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Almasi Kasongo.




Rais wa Klabu hiyo Azimkhan Akber Azimkhan kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.

Mwenyekiti wa Chama cha Soka  mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Almasi Kasongo. Kushoto akizungumza katika mkutano huo.

Hapa wakitiliana saini mkataba huo.






Mkutano ukiendelea.


Hapa mkataba ukiangaliwa baada ya kusainiwa.
Meneja Masoko wa Benki ya Finca, Nicholous John kushoto), akikabidhi jezi kwa Rais wa Klabu hiyo Azimkhan Akber Azimkhan kulia). Wengine kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka  mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Almasi Kasongo na Makamu wa Rais wa Dar City Club, Hamidu Zuberi.

Makabidhiano yakiendelea. 


Na Dotto Mwaibale

Benki ya FINCA Microfinance leo imesaini mkataba wa udhamini  wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 5 na klabu ya soka ya Dar City F.C.

Mkataba huo uliosainiwa jijini Dar es Salaam katika makao makuu ya Benki ya FINCA  , makubaliano hayo yanajumuisha   kuipatia  jezi za michezo klabu hiyo  pamoja na kuipatia timu  fedha za usafiri  na mahitaji mengine ya msingi katika msimu ujao wa ligi Daraja la Pili.

Akizungumza katika hafla ya kusaini makubaliano Meneja amasoko wa FIINCA, Nicholous John  alisema kwamba udhamini huo ni kuthibitisha tena  sera ya benki hiyo ya kujikita katika kusaidia wajasiriamali vijana, kuhakikisha  wanakua na  waje kuwa watu waliofanikiwa  katika sekta ya kifedha na hali kadhalika katika jamii kwa ujumla.

 “FINCA tunaamini katika kukuza  umuhimu wa kukuza uchumi  ndani ya jamii, hususani vijana, na ndio maana  tulikuwa tayari  kukubaliana na juhudi za ziada  za vijana hawa  baada ya kubaini kwamba wanavyo vipaji vya kuwawezesha kufika mbali  kulingana na hali ya michezo ilivyo,” alisema John  na kuongeza kwamba  wameamua  kujumuisha utamaduni wa ujasiriamali katika michezo.

Dar City FC ambayo ilifanikiwa kuingia katika mashindano ya Kombe la Mabingwa wa Shirikisho  hivi karibuni inatarakiwa kusafiri hadi Kahama, mkoani  Shinyanga  ambako itaungana na  timu nyingine saba katika ligi ya mabingwa wa mikoa  nchini.

Aidha Rais wa Klabu hiyo Azimkhan Akber Azimkhan aliishukuru FINCA kwa ukarimu huo wa msaada akisema kuwa  umekuja wakati sahihi na katika kipindi ambacho klabu hiyo  inakabiliwa na changamoto za kifedha.

“Tunatoa shukrani nyingi kwa Benki ya FINCA kwa msaada huu uliokuja kwa wakati mwafaka, sasa hivi tuna uhakika kwamba tutafanya vizuri katika mashindano  kwa kuwa udhamini huu utatuwezesha  kwa kiwango kikubwa kwa timu kuwa na morali  na hamasa  ya kufanya kazi kwa bidii, “ alisema Azimkhan.

 Alifafanua kuwa matayarisho kwa ajili ya mashindano hayo  yanajumuisha mahitaji kadhaa  na  hiyo ni changamoto kwa makampuni mengine, watu binafsi  na mashirika katika kuzisaidia timu zinazoibua  kwa kutambua umuhimu wake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Soka  mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Almasi Kasongo wakati akiishukuru FINCA kwa udhamini wake  alitoa wito kwa taasisi nyingine  za kifedha  kuiga mfano maridhawa wa FINCA  kwa kuzisaidia klabu nyingine za soka zinazoibukia  ndani ya jiji.