Muungano mkuu wa upinzani nchini Kenya, ambao ulishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, umeapa kuendelea na maandamano wenye nia ya kubatilisha kile ambacho unasema kuwa, matokeo "feki" ya uchaguzi mkuu.

Mpinzani mkuu wa Bw Kenyatta, Bw Raila Odinga, amedai kuwa uchaguzi huo ulikumbwa na wizi mkubwa wa kura.
Seneta James Orengo ameiambia BBC kuwa chama chake, kinachoongozwa na Bw Raila Odinga, hakitapinga matokeo ya uchaguzi mkuu mahakamani, huku akisema kuwa Uhuru Kenyatta tayari ametoa vitisho kwa majaji.
Kufikia sasa watu 11 wameuawa katika ghasia za baada ya uchaguzi mkuu, ambazo zilianza mara tu baada ya Uhuru Kenyatta kushinda kutangazwa mshindi kwa muhula wa pili mnamo usiku wa kuamkia Jumamosi.
Tume ya taifa ya kutetea haki za kibinadamu nchini Kenya, imetoa orodha ya juu ya wahasiriwa wa ghasia hizo huku ikisema kuwa ni watu 24 ndio ambao wameuwawa katika visa vinavyohusiwa na uchaguzi huo, huku ikiongeza kuwa polisi wanatumia nguvu kupita kiasi.
Uhuru Kenyatta kushoto) na Mpinzani wake Raila Odinga (kulia)
Image captionUhuru Kenyatta kushoto) na Mpinzani wake Raila Odinga (kulia)
Kaimu Waziri wa usalama wa ndani, Fred Matiangi, amewataja waandamanaji kama "wahalifu".
Kiongozi mmoja mkuu wa chama cha upinzani, Bwana Johnson Muthama, amesema kuwa polisi wanajaribu kuwalazimisha watu "wakubali matokeo hayo."
Mwanamke akijikinga KiberaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionGhasia zilitokea pia mtaa wa Kibera, Nairobi