Watanzania waishio Washington DC na Vitongoji vyake, siku ya Jumapili Jan 14, waliweza kufanya maamuzi ya kuifufua tena Jumuiya ya Watanzania DMV, ilivunjika kwa zaidi ya miaka miwili hadi kufikia kufanya maamuzi ya kuifufua tena upya Jumuiya hiyo.

Kamati ya Maandalizi pamoja na waTanzania waliohudhuria katika mkutano huo, waliweza kufanya maamuzi ya kuteuwa watu saba kuwa ndani ya Kamati ya Uchaguzi, ili kushindikiza katika uchaguzi kujachua viongozi wapya watakaojitokeza kuchukua fumu za kugombea uongozi wa Jumuiya hiyo.

Viongozi wa Kamati ya Mda ya Uchaguzi waliochaguliwa na Watanzania waliohudhuria katika mkutano huo ni ; Robert Saulanga - Mwenyekiti Richard Mawenya - M/Kiti Msaidizi Julius Manase - Katibu Eddha Ghachuma - Muweka Hazina Mama Mushala - Mjumbe Kenyatta - Mjumbe Simba Sakapala - Mjumbe.




Mkutano Mkuu Wakuifufua Upya Jumuiya ya Watanzania DMV