Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na viongozi wa vikosi vya operesheni Nzagamba na Sangara ,ambapo amewataka viongozi kusimamia sheria na miongozo ya  kukusanya maduhuli ya serikali.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)



Timu ya operesheni Sangara,Nzagamba wakiendelea na ukaguzi katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, amewataka viongozi wa vikosi vya operesheni Nzagamba na Sangara, kusimamia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya ya kukusanya maduhuli ya serikali.




Akiwa kwenye ziara yake kwa nyakati tofauti katika ukaguzi wa operesheni hizo kwa mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Mwanza, Ulega alisema wapo wanaokiuka taratibu na miongozo.


Awali mkuu wa timu ya operesheni mkoa wa Singida, Nankondo Senzila, alisema wanaendelea katika kanda hiyo ambapo kazi kubwa ni kukagua mazao ya uvuvi yanayosafirishwa kwenda sehemu mbalimbali


Akiwa Shinyanga, Waziri Ulega alikutana na kuzungumza na timu ya operesheni Nzagamba inayosimamia mikoa ya Tabora na Shinyanga, aliitaka timu hiyo kujijenga vizuri katika kila idara ili kuongeza ukusanyaji wa maduhuli na kuondokana na ujanjaujanja.


Kiongozi wa timu hiyo, Rogers Shengoto alisema katika operesheni hiyo ya mifugo awamu ya pili .Akiwa Mwanza alikutana na timu ya operesheni Nzagamba ya mikoa ya Mwanza na Mara ikiwa kazini na kuwataka wafanye kazi kwa kufuata sheria na kuachana na njia za ujanja zitakazofikia kupungua kwa ukusanywaji wa mapato

Kiongozi wa operesheni wa mikoa hiyo, Shilagi Masele alimweleza Ulega kuwa kwa wiki ya kwanza walipata changamoto ya baadhi ya Halmashauri kutokuwa na tozo mpya katika sekta ya mifugo ambapo walihakikisha wanazijua vizuri na kwa sasa kazi zinaenda vizuri.