Serikali ya Kenya imetuma timu kuchunguza ajali ya helikopta iliyoua mkuu wa jeshi Jenerali Francis Ogolla na wengine tisa.

Haijabainika mara moja kilichosababisha ajali hiyo.

Jenerali Ogolla alikuwa miongoni mwa watu 12 waliokuwa ndani ya ndege hiyo ya kijeshi iliyoanguka Alhamisi alasiri muda mfupi baada ya kupaa kaskazini-magharibi mwa nchi.

Miili ya waliofariki ilisafirishwa hadi Nairobi na manusura wawili wamelazwa hospitalini kutibiwa.

Akitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa, Rais William Ruto alisema vifo hivyo ni "wakati wa huzuni kubwa" kwa nchi.

b
Image caption: Jenerali Ogolla aliteuliwa kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Kenya mwezi Aprili mwaka ja

Bw Ruto alimtaja mshauri wake mkuu wa kijeshi kuwa afisa shupavu aliyefariki akiwa kazini.

“Nchi yetu imempoteza mmoja wa majenerali wake shupavu, maafisa shupavu, wanaume na wanawake wa huduma,” Bw Ruto aliambia taifa.

Jenerali Ogolla alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Kenya kwa mara ya kwanza tarehe 24 Aprili 1984, kulingana na tovuti ya wizara ya ulinzi ya Kenya.

Alitarajiwa kuadhimisha miaka 40 katika jeshi wiki ijayo.