Alipoulizwa na mwandishi wa BBC Jessica Parker kwa nini anakataa kujadili matukio mara moja, waziri wa mambo ya nje wa Marekani Blinken

Alisema kwamba atakuwa "mchoshi sana", kama njia ya mwanadiplomasia huyo mkuu wa Marekani ya kukataa kuzungumzia shambulio la wazi la Israel dhidi ya Iran.

Blinken amesema kwamba Marekani "haikuhusika" katika operesheni yoyote ya kijeshi na inaendelea kufanya juhudi za kwa ajili ya kuhakikisha pande mbili zinapunguza kasi ya mzozo.

Katika kujibu swali la pili kuhusu jinsi atakavyoonyesha hali ya sasa ya mahusiano ya Marekani na Israel, Blinken amesema "tunazungumza mara kwa mara, kila siku".

"Tumejitolea kuisaidia Israel kujilinda na kama ni muhimu kushiriki katika utetezi wake, kama ulivyoona siku chache zilizopita."