Antonio Guterres - katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa - anasema ni "wakati mwafaka wa kukomesha mzunguko hatari wa kulipiza kisasi katika Mashariki ya Kati", kulingana na taarifa kutoka kwa msemaji wake.

Anaongeza kuwa Guterres "analaani kitendo chochote cha kulipiza kisasi na anatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kufanya kazi pamoja ili kuzuia maendeleo yoyote zaidi yanayoweza kusababisha madhara makubwa kwa eneo zima na kwingineko".